Mwili wote unalingana na maisha ya majini. Nyangumi wanaotupwa kwenye nchi kavu wanakufa haraka; wanakauka, uzito wa mwili unagandamiza mapavu kwa sababu wanakosa ueleaji wa maji.
Hata hivyo muundo wa mwili bado ni sawa kama mamalia wengine:
- wanapumua kwa kutumia mapafu; kutegemeana na spishi zinaweza kuzama na kukaa chini ya maji kuanzia dakika kadhaa hadi masaa mawili.
- Huwa na moyo yenye vyumba viwili inayoweza kusambaza oksijeni mwilini kote.
- Nyangumi huwa na damu moto yaani wanaweza kutunza halijoto ya wastani mwilini tofauti na samaki wanaobadilika halijoto ya mwili kulingana na halijoto ya mazingira.
- Wanazaa watoto waliokamilika tayari na kuwanyonyesha maziwa yenye mafuta mengi kwa kutumia viwele vyao. Kiinitete hukua mwilini hadi kuwa mnyama kamili jinsi ilivyo na mamalia wengi.
Mara nyingi spishi za nyangumi zinatofautishwa kutokana na meno yao:
- wale wanaovinda samaki au wanayama wakubwa wengine wa bahari wana meno ya kawaida.
- wale wanaokula planktoni (viumbe vidogo sana baharini) hawana meno bali mifupa ya kinywani ambao si mifupa ya kweli inaundwa na kitu kinachofanana na kucha za vidole. Mifupa hii inakaa kama meno ya chanuo inafanya kazi ya filta; nyangumi huyi anafungua mdomo na kujaza nafasi maji pamoja na yote yaliyomo kama uduvi wadogo sana; ulimi unasukuma maji kupitia chanua ya mifupa ya kinywani na windo unabaki ndani kama chakula.
Himaya: | Animalia (Wanyama) |
Faila: | Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni) |
Ngeli: | Mamalia (Wenye viwele wanaonyonyesha wadogo wao) |
Ngeli ya chini: | Eutheria |
Oda ya juu: | Laurasiatheria |
Oda: | Cetacea (Wanyama kama nyangumi) |
0 comments:
Post a Comment