Friday, February 26, 2016

KUOTA UPALA/UWALAZA- FAHAMU CHANZO NA TIBA YAKE


Siku hizi ni jambo la kawaida sana kuona vijana wa umri wa miaka 20 hadi 35 wakiota Upara. Fanya uchunguzi mdogo tu huko mitaani utagundua vijana wadogo haswa wa kiume wanaota vipara mapema sana kuliko kawaida. Na wengi tunaamini kuwa Upara ni ishara ya busara ama kufanikiwa kimaisha. Leo katika makala hii utaweza kufahamu nini chanzo cha upara katika umri mdogo na ni nini tiba yake. ningependa kukuhakikishia mapema kuwa tiba ipo na haina gharama yoyote.
kikawaida kwa binadamu yeyote iwe mwanamke ama mwanaume huanza kupoteza nywele kichwani kwa kasi kuanzia miaka ya 50 na kuendelea kutoka na kuchoka kwa mwili. Ni swala linalokasirisha sana kwa kijana mdogo kuota upara angali bado unazihitaji nywele.
Haikubaliki
Upara ukuingiapo huanza taratibu taratibu, mwanzoni huwezi kugundua kuwa ni upara unaokunyemelea, utahisi ni matatizo madogo madogo tu ya nywele. kwa mtu ambaye hana kawaida ya kuchunguza nywele zake kwa ukaribu itaweza kuchukua miaka 2 au zaidi kugundua tatizo.
Inafka wakati nywele zinakuwa zimepukutika kwa kiasi kikubwa sana ndipo untambua kwamba hiki ni kipara. inakela sana na usiombe uwe na kichwa chenye umbo baya, uzuri wa sura wote hutoweka na utatamani hata uvae vigi ama ushonee wiving. Ukifikia pointi hii ndipo utapogundua kuwa nywele ni muhimu sana na ni urembo tosha wa binadamu.
Kwa mtu ambaye hajapatwa na hili tatizo hawezi kuona uzito wa hili swala, nina imani vipara vinawakela wengi sana. Na ni vijana wachache sana walio huru na vipara vyao, nao ni wale tu wenye vichwa vyenye umbo zuri ama ni wale wasiojari muonekano wao. Kundi lililobaki wote wanatamani miujiza itendeke vichwa vyao viweze kuotesha nywele tena..
Nadhani leo ni nafasi nzuri kwako kufahamu ni nini chanzo cha vipara kwa vijana wenye umli mdogo na namna ya kutibu. zipo sababu nyingi sana. na kwa kijana yeyote iliye na upara atakuwa amekumbwa na sababu moja wapo ama mbili kati ya hizi nitakazo kueleza
CHANZO/SABABU ZA KUOTA UPALA KATIKA UMRI MDOGO
Lishe duni,
Nafasi kubwa ya nywele imajengwa kwa protini, pia kuna virutubisho vingine vingi vinavyosaidia uzalishaji wa nywele, kama madini ya zinki, chuma, potasiamu, vitamin E, B, C na hewa ya oksigeni. virutubisho hivi tunavipata kutokana na vyakula tunavyokula kila siku. baada ya kuliwa, virutubisho hivi husambazwa kwenye ngozi ya fuvu la kichwa (Scarp) kwa njia ya damu. Mtu yeyote akikosa virutubisho hivi kwa kiwango kinachotakiwa lazima atapatwa tatizo la kupukutika kwa nywele.
Tambua kuwa madawa na mafuta mengi ya nywele tunayoyatumia hutengenezwa kwa tutumia vyakula vyenye virutubisho hivi, hakuna uchawi mwingine. Katika Makala ijayo nitakueleza kwa undani zaidi ni vyakula gani unavyopaswa kula ili uweze kuwa na nywele nzuri, wala hakuna haja ya kuhangaika na madawa.

Msongo wa Mawazo. (Stress),

Msongo wa mawazo ni chanzo king I one kikubwa sana cha tatizo la nywele na ndicho haswa kinachowakumba vijana wengi wa sasa na kuwasababishia vipara katika umri mdogo. Kitaaramu imegundulika kuwa msongo wa mawazo unaathiri mzunguko wa damu kwenye ngozi ya vuvu la kichwa hivo damu hushidwa kufikisha virutubisho na hewa ya kutosha kwa ajiri ya uzalishaji wa nywele.
Kikawaida binadamu anapokuwa anawaza sana misuli iliyozunguka fuvu la kichwa kusinyaa na kukunjamana kitu ambacho husababisha ngozi na mishipa midogo midoho ya damu kusinyaa na kukunjamana pia hivyo damu inashidwa kupenya na kusambaa kwa urahisi katika maeneo yote ya ngozi ya kichwa kitu kinachopelekea upungufu wa virutubisho na hewa kwa ajili ya ukuaji wa nywele na hatimaye nywele huanza kudhoofika. baadhi ya wasomi na watu wanaopigana sana na ugumu wa maisha hupata vipara kwa njia hii.
Matatizo katika mfumo wa homoni,

Homoni zinahusika sana na kukuaji wa nywele. Upugnufu ama madiliko katika homoni husababisha kudhoofu kwa nywele, kuna sababu nyingi zinazoathiri mfumo wa homoni, mfano Magonjwa, Ujauzito, mwili kukosa hewa ya oksigeni yakutosha pamoja na uvutaji wa sigara.
Kurithi toka kwa wazazi,
Pia inaaminika bainadamu anaweza kurithi tatizo la upara kutoka kwa kizazi chake kilichotangulia. Lakini hapa huwa najiuliza sana sabubu kuna baadhi ya watu wamepata vipara wakati kwenye ukoo wao hakujatokea mtu mwenye upara.
Baada ya kufahamu chanzo cha upara, Sasa unahitaji kufahamu namna ya kutibu tatizo.
Najua niechukua muda wako mwingi sana kuipitia makala hii lakini naamini umejifunza kitu. Katika makala nitakayokuandalia kesho ilazungumzia kiundani namna ya kutatua tatizo la upara.kwa leo inatosha najua utachoka kusoma. Nakuhakikishia kuwa kutibu upara inawezekana tena kwa kutumia vyakula na dawa zetu za asili ambazo naamini zinapatikana katika kila nyumba hapa kwetu Tanzania. Nitakueleza namna ya kutengeneza dawa hizi. Zimewasaidia wengi ingawa bado hazijafahamika sana.

0 comments:

Post a Comment