Friday, February 19, 2016

Anasa za kidunia

Kijana wa kiume alimwambia baba yake "nimemuona msichana mzuri sana na ninataka nimuoe hivi karibuni. Ni mzuri sana na ana macho mazuri mno" baba akamwambia sawa mwanangu mlete nyumbani umtambulishe.
Kijana alimleta yule msichana nyumbani, baba alikubali uzuri wa yule binti na kumwambia mwanae "mwanangu hustahili kuwa na msichana huyu. Binti kama huyu anastahili kuwa na mtu mwenye uzoefu wa maisha na anayeweza kumtegemea. Mtu kama mimi"
Kijana alishangaa msimamo wa baba yake na akamwambia "nitamuoa mimi na sio wewe baba" na ghafla wakaanza kugombana, na baadae wakaamua kwenda police kusuruhisha.
Walipomuelezea afisa wa polisi tatizo lao, yule afisa akawaambia wamlete huyo msichana kwake wamuulize yeye anamhitaji nani. Afisa alipomuona yule msichana akawageukia baba na mtoto na kuwaambia "wote ninyi hamfai kuwa na msichana huyu, anahitaji mtu aliye juu kama mimi, mtu ambaye ana nguvu za kuweza kumlinda."
Wote watatu wakaanza kuzichapa, na baadae mkuu wa kituo akatokea. Mkuu wa kituo akawauliza wanagombania nini na wote kwa pamoja wakamuonesha mkuu wa kituo yule binti. Mkuu alipomuona binti akawaambie "nyie wote ni wapumbavu, msichana mzuri kama huyu afaa kuwa mke wa mkuu wa kituo! Ondokeni hapa na mniachie huyu binti niongee nae"
Wote wanne wakaanza kugombana tena, mwishoni yule binti akawatuliza na kuwaambia "me nina ufumbuzi wa huu mgogoro wenu nitaanza kukimbia, yeyote atakayefanikiwa kunikamata atakuwa mme wangu" alipoaanza kukimbia wote wanne wakaanza kumfukuzia ili kumkamata ma ghafla wote wanne wakatumbukia katika shimo kubwa.
Binti akawatazama tokea juu ya lile shimo na kuwaambia "mnajua mimi ni nani? Mimi ni ulimwengu huu. Watu wanakimbia kweli kunikamata au kwenda sambamba na mimi, kwa kufanya hivyo wamemsahau hata Mungu mpaka pale wanapoingia kaburini wamekufa bila ya kuweka uhusiano mzuri na Mungu! Yote ni kwa ajili ya uzuri tu wa mimi! Nawaambieni tu Mungu yupo! Msitazame uzuri wa ulimwengu huu mkamsahau Mungu.
Muhimu.
Usimsahau mwenyezi Mungu, anakupigania unapumua mpaka leo hii, usizubaishwe na anasa za ulimwengu huu! Mfalme Sulemani alisema vyote ni ubatili mtupu.
Kwanini usiseme AMEN!??

0 comments:

Post a Comment