Thursday, March 21, 2013

MTU KWA MTU KUHUSU NGONO!.


MTU KWA MTU KUHUSU NGONO

       Mpenzi naomba ufanikiwe katika mambo yote na kuwa na afya kama vile roho yako ifanikiwavyo” 3Yohana 2.  Nilipotembelea Norhlea shule ya secondary ya wavulana huko Bulawayo, hili ndio lilikuwa fungu la mazungumzo yangu. Wengi wa vijana wanapita na ushindi wa juu kwa makusudi ya kufanikiwa maishani, lakini kama hawajizoezi kuepuka uasherati hawawezi kuishi muda mrefu ili kutimiza malengo/ndoto zao.  Kuna vitisho dhahiri kwa watoto wanaokua katika kipindi hiki cha historia.  Kuenea kwa UKIMWI kumekuwa tishio kiasi kwamba mtoa kodi wa Zimbabwe anakatwa aslimia 3% ya mshahara wake ili kusaidia kuchangia swala la UKIMWI. Kwa furaha ya muda mfupi, wengi wamechezea kamari furaha yao ya baadaye na umaarufu wa maisha yao. Kinachohitajika  kwa Kijana ni kuongozwa na kanuni kuliko msisimko. Je, Mungu ametupatia faida sisi vijana kufanya maamuzi maishani mwetu? Mungu katika Busara yake aliumba wanaume kama viumbe wenye akili. Hii ina maana kuwa ikiwa linaleta maana tutalifanya. Wanawake wana hisia za haraka, kama inaonekana vema watalifanya. Haileti maana kuweka tumaini lako katika kondomu.
         Sio uungwana kumpa msichana mimba wakati hujamwoa. Sio salama kutumaini silica yako ukiwa kwenye nchi ambayo mmoja katika kila watu wane ana virus vya UKIMWI 1/4. Ili kuweza kufuata kanuni kwa msimamo thabiti, inampasa kila mtu ajielewe na ajithamini.
Jifahamu wewe u nani?.
        Shetani amejaribu kutuondelea haki na uthibitisho wa kujielewa na kujifahamu nafsi zetu tangu mwanzo.  Kufahamu sisi ni akina nani ni msingi wa kutenda kulingana na mapenzi ya Mungu na sio shetani, “Wapenzi sasa tu wana wa Mungu.” Kwa vile Mungu ndiye mtawala wa Ulimwengu, lazima tuwe wana wa Kifalme. Tumepangiwa mafanikio makubwa. Kila mmoja wetu anazo angalau chembe chembe  za fahamu billion 17 kwenye ubongo wetu. Kila chembe ina uwezo wa kushughulikia aina mia mbili za habari. Wasomi wetu wametumia sana sana 10% tu ya uwezo wa ubongo wao. Kama kipaumbele cha maisha yako ni sahihi, unaweza kujumuishwa kwenye kundi hili dogo la wenye uwezo mkubwa wa ubongo. Shetani amejaribu kuzuia fikara zetu ili tusiweze kufikiria chochote kiwezacho kutufanya tufanye bidii ili kupata mafanikio ya kweli.
        Fikiria! Ni nini nitakalo ili nifanikiwe katika maisha yangu? Ni vikwazo gani vimewafanya wengine washindwe katika kujaribu kwao? Mimi nitaviepukaje?
        Katika kugundua wewe ni nani, soma vitabu ambavyo vitakusaidia kuelewa mwenendo wa binadamu. Biblia/Quran ndiyo vya kwanza na muhimu sana. Ndivyo vitabu pekee vinavyotoa taarifa yenye mamlaka ya namna ilivyofanyika tukawa Hai. Watu wengi wamebadilishwa kutoka katika tabia za kuwa wanyama au maharamia na kuwa watu wanaofanana na Kristo/Mtume kwa kujifunza vitabu hivi. Juhudi ya roho ya kinyama haiwezi kutawala mwanadamu ambaye anajifunza Biblia/Quran kwa dhati.

Jipe nafasi.
      Watu wengi husikiliza vitu vyote ambavyo ni kinyume vinavyozungumzwa kuwahusu na kuishia kusema pia mambo hasi kuhusu hao wanaomsema. Wote tunayo haki tulivyo. Tunahitaji kutambuliwa kwa mchango wetu wa namna ya pekee kwa jamii ya binadamu. Muumini wakati mwingine hujiingiza katika ngono kabla ya ndoa kwa sababu ya kujiona kuwa ana mwonekano hafifu. Hivi sivyo Mungu alivyotuumba, bali mazingira yanavyotukuza.
       Utafiti wa wanasaikolojia Fulani ulionyesha kuwa, tabia ya watu kujisikia bora, kujiamini katika mwonekano kulishuka kutoka 70% mtu akiwa na miaka mitano(5) hadi 2% katika maisha ya awali ya utu uzima. Ni wale tu walio na elimu ya kujifahamu wao ni akina nani na wanaojikubali wao wenyewe, watakuwa tayari kupokea na kukabili mambo ya hasi dhidi yao.
       Yusufu alipata uzoefu mkubwa wa kukatisha tamaa wa kuuzwa utumwani, lakini alijipa nafasi ya kuishi na ndoto zake na hatimaye akawa waziri mkuu wa Misri. Aliweza kuvumilia majaribu ya mwanamke mrembo, ingawa ilimgharimu kwenda gerezani.


Wewe ni wa namna ya peke yako.
      Bahati ya kupata mtu mnayefanana kabisa ulimwenguni ni ndogo sana, kama moja kwa milioni mia tatu(3ml). Una mchango wa pekee wa kutoa katika maisha haya.
      Kwanini ufe kabla hujawakilisha mchango wako? Epuka kuzurura au kuhusiana na watu ambao hupendezwi na viwango vya maadili yao..
      Moyo wa mwanadamu ni mnyonge, dhaifu na hauaminiki, tunavutiwa kwa nguvu zaidi na mazungumzo ya kinyama tunayoyasikia kuliko yale ya kweli. Wakati mwingine ni muhimu kuorodhesha mambo unayoyapenda kukuhusu wewe mwenyewe. Wakati unapojisikia umechukizwa na kukata tamaa, chukua orodha yako na uisome kwa sauti. Vijana wanaokwenda kwenye nyumba za ibada wana nafasi nzuri ya kuzungukwa na vijana marafiki wanaowachangamsha. Hivyo wanafikiria zaidi kuhusu masuala ya uzalishaji. Jipatie nafasi..

Acha ndoto zako zitimie.

Uwe na lengo maishani.
      Kuishi maisha yasiyo na malengo maalum ni hasara na kuishi kusikofaa. Kila mtu inampasa awe na kusudi maalum la wazi maishani mwake. Kama hujui unachotaka kufanya na maisha yako, tafuta washauri wenye busara kuliko wewe wakusaidie. Maisha bila lengo hushusha hadhi zetu na kutufanya tusiwe na tofauti na wanyama. Sishangai watu wengi wana tabia kama za wanyama, wakitawaliwa na tamaa zao.
      
Ondoa Giza.
      Thomas Edson alipokuwa anagundua mwanga wa balbu, hakuna ambacho kingemzuia kufanya hivyo. Mama yake aliambiwa na mkuu wa shule kwamba hatafanikiwa sana na mara kwa mara alimruhusu akauze magazeti. Magazeti haya yalikuwa na taarifa za ugunduzi wa karibuni na hivyo zikajenga katika moyo wa Thomas shauku ya kugundua kitu Fulani. Usiku aliweza kwenda maabara kufanya jaribio moja baada ya jingine. Baada ya majaribio mengi mama yake alijaribu kumkatisha tamaa kwa kusema alikuwa anapoteza muda. Hata hivyo Thomas alimjibu kwamba japo hadi wakati alikuwa hajafanikiwa, lakini moja ya jaribio litafanikiwa kwa hakika. Muda mfupi baada ya hapo, Thomas Edson akagundua mwanga wa balbu
     Lengo ni kitu ambacho kinakuchochea kuwa na ari ya juu kiasi kwamba hata mama yako hawezi kukuzuia kukifanya, Watu wengi wamefanya majaribio kulewa, Madawa ya kulevya na ngono, na vyote hivi havikuwaletea furaha ya kudumu. Una bahati na faida ya kuelewa ni majaribio gani hayafanikiwi. Kwa nini ufanye uchaguzi wa kipumbavu…..!!!
      Wenye busara hujisahihisha wenyewe kutokana na makosa ya kipumbavu waliyoyatenda.

Lenga mbali.
      Lengo kuu ambalo kila Mwanadamu anahitaji kulifanya katika maisha ni kuongozwa na kanuni na sio hisia. “Kusalimisha uwezo wetu wote kwa Mungu hupunguza sana matatizo ya maisha.” Inadhoofisha na kufupisha maelfu ya masumbufu na tamaa za asili za moyo.” Messages to young Lovers”. UK. 63, Ellen White

Tamaa za asili za moyo:
      Kando ya kujizuia kufanya ngono na wasichana, kijana wa kiume akubaliane na matukio machache ambayo yamekuwa wazi. Wakati wa kuandaa kuandika makala hii, kijana mmoja kutoka shule ya sekondari aliniomba nijumuishe habari kuhusu ubasha au ushoga na punyeto.

Ubasha na Ushoga.
       Wazimbabwe wengi hawafikirii hili kuwa tatizo kubwa, hivyo utafiti kidogo sana umefanywa kuhusiana na swala hili. Kwanza hebu tuweke wazi misimamo yetu, tunaamini kwamba ubasha au ushoga umelaaniwa katika Biblia Yuda anaelezea hili kuwa moja ya sababu kwa nini Mungu aliadhibu Sodoma na Gomora. Yuda 7:8, Paulo alikiita kitendo hiki kuwa sio cha kawaida na alikilinganisha na kiumbe badala ya Mungu. Hata Rais Mugabe amekemea na amelaani kitendo hiki kwa kusema kwamba sio cha Kibiblia au kiafrika. Kwa mara ya kwanza nilipokutana na matendo ya ubasha na ushoga ilikuwa kwenye shule ya misheni kama kilometa 28 nje ya Harare. Mkuu wa Bweni wa shule hii alikuwa anawapanga wavulana mstarini na kuchagua wote waliokuwa na mwonekano wa sura nzuri. Baada ya hapo aliwapangia kufanya kazi nyumbani kwake. Kuna wakati mwingine aliwabusu hawa wavulana na huenda hata kulawiti. Alikuwa ameoa mwanamke jeuri na anayemtawala kiasi kwamba wakati mwingine alimpiga mumewe.
       Nadharia nyingi zimeendelea kuelezea kwa nini watu wngine wamechagua uhusiano wa ngono ya ubasha au ushoga kuliko ule wa mke na mume. Katika utafiti wangu nimetambua kwamba wengi wa mabasha au mashoga watakuwa hivyo kutokana na uhusiano wao na rafiki wanayemwamini, kiongozi au jamaa. Hata katika nchi zinazovumilia mambo kama haya kama ulaya, ubasha au ushoga haufikiriwi kuwa sahihi kwa 66% ya wanaume na 50% ya wanawake. Huko Zimbabwe 99% ya watu wanauona Ubasha au ushoga ni mbaya. Uhusiano wa kulawitiana kwa wanaume unasemekana kuwa na maumivu na uchungu, lakini wengi wanaendelea na hivyo kwa vile wanasisimuana hadi kufikia mshindo. Baadhi ya mabasha au mashoga, wanapenda kuwa na uhusiano wa ngono wa kawaida kati ya mke na mume. Unakuta wana mke na watoto, lakini bado wanapendelea kufanya ngono na wanaume wengine. Magonjwa ya UKIMWI na Heapatitis B ni tishio la afya kwa mabasha na mashoga.

Punyeto.
      Unakumbuka kuota kuhusu picha au sinema ya ngono halafu unakakamaa kabla hujajua kuwa nguo yako ya ndani imelowana?  Vijana wengi hupitia uzoefu huu. Mamlaka ya Australia inaamini kuwa hadi 90% ya wavulana wanapitia uzoefu katika maisha yao, na 10% wanaosema hawakupitia ni waongo. Je, ndoto nyevu zinatokeaje? Wakati homoni au vichocheo vinapotolewa, mbegu za kiume hujaza ndani ya mirija ya kiume (seminal vesicles). Mirija hii ikijaa, mwili hujaribu kuzitoa na njia ya kawaida ya kuzitoa ni kwa njia ya ndoto nyevu.
     Hii yenyewe sio kosa kwa vile ni hatua ya Kibayologia, lakini inaweza kujenga tabia ambayo ina madhara na ni dhambi kwa Mungu. Punyeto au ngono binafsi hudhihirisha udhaifu kwa kijana ambaye hufinyafinya, hushikashika au kuchezea viungo vyake vya kiume ili kujitimizia haja ya ngono na kufikia mshindo. Hii sio kitu kinachofanyika bila mtu kuwa na fahamu bali hufanyika mtu akiwa na fahamu kamili.  Punyeto ina madhara kwa vile inawashawishi vijana kutafakari kuhusu ngono na kuondoa mawazo ya kutafakari kuhusu mambo mengine muhimu.  Kazi za shule zitaathirika kwa mazoea haya.

P.E
     Tatizo kubwa la punyeto ni kutoa mbegu za kiume kabla ya kufikia mshindo. Watu wengi huchukua hata dakika kumi(10) kabla ya kutoa mbegu za kiume wakiwa wanatenda tendo la ngono, lakini katika hali ya punyeto mbegu za kiume hutoka kabla ya mshindo sekunde chache baada ya kitendo kuanza.  Wanawake wengi hawawezi kuvumilia hali ya aina hii mpaka kifo kiwatenganishe wakiwa pamoja.  Kila mmoja ana haki kwa mwenzake kumfanikisha katika tendo hili, hivyo usimkatalie mwenzi wako wa baadaye kile ambacho anapaswa kukipata kwako. Kufanya mapenzi na mtu wa jinsia yako sio kawaida kwa namna yoyote.
     Kwa hitimisho, napenda kusema kwamba Mungu alituumba kwa namna ya ajabu na hivyo tunatakiwa kumcha kwa kicho. Kama tukifuata mashauri ndani ya maandiko yake katika maisha yetu hatutabadilishwa kirahisi. Ngono si kitu cha kuchangamkia. Kwa wastani waliooana wana miaka arobaini ya kufanyisha viungo vyao vya uzazi mazoezi haya. Kuharakisha zawadi hii, kunaweza kukupunguzia nafasi ya bahati yako njema. Uvumilivu ni maadili na jambo la msingi.










                                                                                               Created by Michael Nyagei Magessa

3 comments: